1 of 37

KF 102 UTANGULIZI WA FASIHI SIMULIZI NA ANDISHI

MODULI YA KWANZA NA YA PILI

2020/21

2 of 37

  • Tunajifunza somo hili ili tugundue nini?
  • Sanaa ni njia ya mwanadamu kujieleza
  • Fasihi kama kioo cha jamii – kinaioneshaje jamii?
  • Lugha kama kioo cha fikra – kinazionesha fikra zipi
  • Lugha kama kichukuzi cha mila – inachukua mila

MALENGO MAKUU YA KF 102

3 of 37

  • Tunakuandaeni muyatimize malengo ya elimu ya CKD kupitia taaluma ya UHAKIKI
  • UHAKIKI WA KAZI ZA KIFASIHI
  • FASIHI YA KISWAHILI
  • Muwe WAHAKIKI
  • Hii ni kozi ya UTANGULIZI
  • Inakupatieni stadi za AWALI na za MSINGI katika UHAKIKI AU UCHAMBUZI wa kazi za KIFASIHI.
  • NI STADI GANI HIZO HASA

MALENGO MAKUU TA KF 102

4 of 37

MODULI YA 1

  • Dhana za msingi
  • Fasihi ni nini
  • Dhima ya fasihi
  • Fasihi ina dhima gani/zipi
  • Je, dhima za fasihi ni za namna moja
  • Chimbuko la fasihi
  • je, fasihi imetoka wapi
  • Mambo gani yamechochea kuibuka kwa fasihi ya Kiswahili

5 of 37

Dhana za msingi

  • Fasihi ni Nini?

1. Etimolojia

  • littera/Kilatini……herufi au uandikaji
  • Literature/Kiingereza
  • Adabu/Kiarabu……ufasaha wa kauli
  • Fusuh/Kiarabu….
  • Fasihi/Kiswahili

6 of 37

2. Mitazamo mbalimbali

Littera,Literature, Adabu/fusuh….Fasihi

  • Uelewa wa watu umekuwa ukitofautiana
  • Kutoka mtu na mtu, kutoka jamii moja na nyingine, kutoka zama hadi zama. kuhusu dhana ya littera, literature, adabu/fusuh.
  • A] jumla ya maandishi katika lugha fulani
  • B] maandishi bora/jamili ya kisanaa yenye manufaa
  • C] sanaa ya lugha yenye ubunifu
  • D] hisi zinazojifafanua kwa njia ya lugha
  • E] matumizi ya lugha kwa njia isiyo ya kawaida

7 of 37

Fasihi ni Maandishi

  • Kila maandishi ni fasihi
  • Fasihi lazima iandikwe

8 of 37

Fasihi ni maandishi bora/jamili

  • Huandikwa na watu bora, nasaba tukufu
  • Sharti yawe ya kisanaa
  • Sharti yawe na manufaa ya kudumu

9 of 37

Sanaa ya lugha yenye ubunifu

  • Yaweza kuwa imeandikwa au la
  • Yaweza kubuniwa na watu wa nasaba/tabaka la juu au la chini
  • Kigezo kikubwa ni kwamba iwe Sanaa yenye ubunifu

10 of 37

Fasihi ni hisi

  • Ni hisi zinazojifafanua kwa njia ya lugha
  • Fasihi yenyewe ni hisi
  • Yaelezwayo na fasihi ni hisi
  • Mtindo utumikao kuelezea hisi ni wa kihisia
  • Sio tu suala la hisia, bali ni uoneshaji wa mahusiano baina ya watu; na watu na dunia yao katika jamii kwa njia ya kisanaa.
  • Fasihi si hisi, bali inaweza kutumia mtindo wa kihisia kuelezea hisia mbalimbali
  • Mfn. Inaweza kuelezea hisia za mapenzi, ila yenyewe sio mapenzi.

11 of 37

Matumizi ya lugha isiyo ya kawaida

  • Fasihi ni Sanaa hasa kwa vile huitumia lugha kwa njia isiyo ya kawaida
  • Uso kawaida

Wasanii hasa wa ushairi hukiuka taratibu za kawaida za matumzi ya lugha ktk sarufi, maana na sauti. [UKENGEUSHI]

  • Athari

Lugha isiyo ya kawaida hutumika ili kuleta athari maalum kwa wasomaji/wasikilizaji. Kutokana na athari hiyo msomaji/msikilizaji huvutiwa na huathirika msomaj. Hatimaye humfanya aitafakari lugha yenyewe badala ya kuutafakari ujumbe tu

12 of 37

lugha isiyo ya kawaida

  • Imesisitiza fani zaidi kuliko maudhui, maana na muktadha uliovyaza kazi ya kisanaa/kifasihi
  • Suala la ukengeushi hujitokeza zaidi katika Sanaa ya ushairi kuliko Sanaa nyinginezo. Sio Sanaa zote.
  • Fasihi huweza pia kuelezwa kwa kutumia lugha ya kawaida.

13 of 37

Majumuisho

  • Fasihi ni Nini?

NI SANAA ambayo hutengenezwa kutokana na mchakato wa kihistoria na kiharakati katika maisha ya jamii.

NI SANAA ambayo usanii wake hujidhihirisha kupitia matumizi ya kawaida, iwe ya kawaida au isiyo ya kawaida

NI SANAA ambayo hujadili maisha kwa kipindi fulani cha historia, historia yenyewe, chimbuko la jambo na mustakabali wake

NI SANAA ambayo huonesha ubora na udhaifu wa jamii mithili ya kioo [fasihi ni kioo cha jamii]. Fasihi ni Zaidi ya Kioo kwani Haituoneshi tu, bali ni mjadala wa harakati za mwanadamu katika kuyaingia maisha, kuyatengeneza, kuyabadilisha, kuyaishi na hatimaye kuachana na maisha

14 of 37

Dhima ya Fasihi

Fasihi hufanya kazi gani

  • Jawabu sahihi kuhusu swali hili hutegemea mambo kadhaa
  • Muulizaji anatoka katika tabaka lipi
  • Kwake huyo muuliza swali Fasihi ni nini

15 of 37

Hii ni kwa sababu Fasihi ni zao la Kitabaka.�A. Tabaka husaidiwa na itikadi katika Kujiimarisha.�B. Itikadi: Mfumo wa mawazo, imani kuhusu mahusiano na maongozi ya watu ktk Jamii

16 of 37

Kwa ujumla, fasihi hutekeleza dhima zifuatazo

  • Kuburudisha
  • Kuhimiza Kazi
  • Kujenga moyo wa kazi
  • Kujenga tabia: Kuonya, Kuasa, Kufunza
  • Kuelimisha
  • Kuhifadhi kurithisha amali za Jamii (mila, desturi, thamani n.k)
  • Kukuza na Kuhifadhi lugha
  • Kuendeleza harakati fulani katika Jamii
  • Ujenzi wa Utaifa
  • Kuleta Ukombozi: Hasa wa kifikra, kisiasa, kiuchumi, kitabaka, kijinsia, n.k

17 of 37

Majumuishofasihi hufanya kazi gani

  • Talii maandiko mbalimbali yahusuyo uhakiki wa fasihi na kisha jadili dhima ya fasihi kwa mujibu wa makundi ya wataalamu/wahakiki wa fasihi wafuatao
  • Wahakiki wa Ulaya hususan Aristotle, Plato, Horace, Karl Marx, na Immanuel Kant.
  • Wahakiki wa fasihi ya Kiswahili hususan Kezilahabi, Msokile na Mulokozi

18 of 37

Chimbuko la Fasihi

Hivi Fasihi ilitoka wapi?

Na Je kila Jamii ina Fasihi au Fasihi ni kwa wachache?

  • Kuna Nadharia au Mitazamo 4
  • IMETOKA KWA MUNGU
  • IMETOKANA NA SIHIRI
  • IMETOKANA NA MWIGO
  • IMETOKANA NA JUHUDI ZA MWANADAMU

19 of 37

I. Mungu/Miungu

i. Fasihi ni Sanaa, Mungu ni msanii mkuu kwa kutumia usanii wake kaumba vitu vyote ikiwemo mwanadamu mwenyewe na Sanaa mbalimbali kama vile fasihi.

ii. Uwezo mwanadamu wa kuumba/kubuni Sanaa kaupewa na Mungu, ambaye ndiye msanii Mkuu.

iii. Fasihi imekuwako duniani tangu kuwepo kwa mwanadamu,

iv. Fasihi ni kama zawadi toka kwa mungu kwa wateule wachache

A] ni ya kidhanifu,

B] inachanganya imani na taaluma

20 of 37

II. SIHIRI

  • Hizi ni uwezo au nguvu za miujiza zinazotumiwa na watu kusababisha matokeo fulani
  • Imani katika miujiza [hapo zamani] ilichukua nafasi ya sayansi na ugunduzi [ya leo]
  • Fasihi na Sanaa nyingine ni haja ya mwanadamu
    • Kujaribu kukabiliana na kuyashinda mazingira.
    • Kuchora, Kuchonga, Kujenga vijumba na kunuizia
    • (SIKU HIZI) Kuombea vitambaa au Kifaa n.k

A] inachanganya dhima na chimbuko

B] ni ya kidhanifu

21 of 37

III. Mwigo/uigaji

    • Etimolojia
    • Mimesis/Kiyunani
    • Mwigo/Kiswahili
    • Imitaion/Kiingereza

2. Maana yake hasa ni kuwa mwanadamu alianza kuwa mbunifu kwa maumbile yaliyomzunguka.

3. Fasihi ni mwigo ukimaanisha uwakilishi wa jambo kwa jingine. Ni taswira inayolenga kuonesha jambo kwa njia ya kufananisha kitu halisi na kisicho halisi.

4. Mwanadamu ni kiumbe wa uigaji, tokea mtoto na aliiga vitu kama vile

    • mazingira, sauti, mwonekano, wanyama, ndege, nk
    • Kubuni hali ya ufanano
    • Ushairi ulichimbuka kutoka ktk kuiga
    • Mwanadamu ni kiumbe wa uigaji, tokea mtoto

22 of 37

IV. Juhudi ya Mwanadamu

  • Chimbuko la fasihi ni Mabadiliko ya Mwanadamu katika kuyadhibiti mazingira yake
  • Charles Darwin aliyeasisi nadharia ya Ubadilikaji Taratibu [evolution theory]. Mwanadamu alikuwa sokwe, na polepole alianza kubadilika na kuwa mwanadamu kamili. Katika mabadiliko hayo alibuni lugha na Sanaa ili kujieleza, kujitambua na kuwaeleza wengine.
  • Udhanifu…..tulikuwa masokwe
  • Uyakinifu…..amebuni Sanaa mwenyewe kutokana na mazingira yanayomzunguka

23 of 37

Juhudi ya Mwanadamu…….

  • Marx na Engels
  • Wanaingalia Fasihi kama zao la mabadiliko katika maisha ya mwanadamu ambayo hutawaliwa na
    • Mfumo wa uzalishaji mali
    • Uhusiano katika uzalishaji mali
    • Mfumo na Uhusiano hutokeza MATABAKA
  • Fasihi ni zao la Matabaka na Uhusiano katika uzalishaji mali
  • Katika uhusiano mwanadamu alihitaji lugha, ambayo ndicho kiini cha fasihi
  • Jamii za wanadamu zimepitia katika mifumo mbalimbali ya kimaendeleo
  • Kwa kila mfumo, kuna vidokezo kadhaa vya kisanaa/kifasihi.

24 of 37

Majumuisho

Tumeona kuwa hakuna fasili moja ya fasihi inayokubalika kwa kila mtu. Kuna mitazamo.

Tumeona pia kuwa watu hutofautiana hata katika kuelezea chimbuko la fasihi. Kuna mitazamo.

Kila mtazamo una uzuri wake na dosari zake. Tunatakiwa tusome kwa makini ili tuzichuje dosari husika dhidi ya uzuri wa mitazamo.

Mara ya mwisho tumesikia kuwa hoja yenye uzito zaidi kuhusu chimbuko ni hoja kwamba fasihi imetokana na juhudi za mwanadamu mwenyewe, na kwamba juhudi hizo zimekuwa zikibadilikabadilika toka jamii/jamii na toka zama/zama

25 of 37

Majumuisho

Tutatumia kielelezo cha maendeleo ya mwanadamu kilichopendekezwa na Marx na Engels

  • Kudadisi upya maana ya fasihi
  • Kudadisi upya chimbuko la fasihi
  • Kudadisi dhima ya fasihi

FASIHI NI ZAO LA HISTORIA

Huiitika historia, na huchongwa na historia.

Tunayafanya haya kwa kujikita katika m,uktadha wa fasihi ya Kiswahili.

Pengine tuanze mjadala wetu na

Dhana yenyewe ya fasihi ya Kiswahili, ndipo tujadili maendeleo yake katika mifumo ya mwanadamu

26 of 37

Fasihi ya Kiswahili�- ni ipi hasa

  • Sengo [1987, 1995]
  • Senkoro [1988]
  • Syambo na Mazrui [1992]
  • Madumulla [2009]
  • Mulokozi [2017]

27 of 37

Sengo [1987, 1995]

  • Waswahili ni kabila au taifa mahsusi la watu waishio pwani ya A.M
  • Watu hao hao wanayo fasihi yao iitwayo fasihi ya Kiswahili.
  • Wengine ambao si wa pwani lakini wanatunga kazi kwa Kiswahili, kazi zoa zaitwa fasihi katika kiswahili

28 of 37

Senkoro [1988]

  • Fasihi X itakuwa ya Kiswahili endapo itajihusisha na kujitambulisha na utamaduni wa Waswahili
  • Waswahili si kabila maalum la watu waishio pwani bali ni watu wa A.M na Kati kwa ujumla wake, sio wale waishio pwani peke yake.
  • Kwa sasa, kabila la waswahili haliko tena.
  • Je, fasihi ya Kiswahili itakuwako, na itakuwa ni ya namna gani

29 of 37

Syambo na Mazrui [1992]

  • Fasihi ya Kiswahili ni ile iliyoandikwa au kutungwa kwa Kiswahili.
  • Inaweza kujadili utamaduni wa mswahili au utamaduni mwingineo
  • Iwe imefuata mbinu za ufasaha wa lugha ya Kiswahili
  • Ni fasihi yote iliyoelezwa kwa lugha ya Kiswahili.

30 of 37

Madumulla [2009]

  • Kuna dhana mbalimbali za Mswahili
  • Dhana ya kijadi kwamba mswahili ni mwanajamii wa kundi au taifa Fulani mojawapo la wenyeji wa upwa wa A.M na visiwa vyake kama vile Waamu, Waunguja, Wapate
  • Dhana ya kisiasa kwamba mswahili ni Mtanzania yoyote. Dhana hii iliibuka miaka ya 1970
  • Dhana ya Uarabu kwamba mswahili ni Chotara.
  • Fasihi ya Kiswahili ipo, na inajumusha fasihi yoyote iliyoelezwa kwa lugha ya Kiswahili. Fasihi hiyo huzalishwa na makundi 4 ya wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili.

31 of 37

Makundi 4 ya wazungumzaji wa Kiswahili

  • Waswahili kindakindaki; wazazi wao wote ni Waswahili
  • Waliohamia bara kutokea pwani, wanatokea kwa Waswahili wa pwani
  • Hawadai kuwa wao ni waswahili, bali huendesha shughuli zao kwa Kiswahili.
  • Watoto wanaozaliwa, kulelewa na kukuzwa katika mazingira ambamo Kiswahili peke yake ndicho kinachotumika katika shughuli za maisha ya maisha yao

Wazalishaji wa fasihi ya Kiswahili

32 of 37

Mulokozi [2017]

  • Kitambulisho kikuu cha fasihi ya Kiswahili ni lugha ya Kiswahili.
  • Kuna ruwaza 3 za fasihi ya lugha ya Kiswahili
  • fasihi ya Waswahili,
  • fasihi kwa Kiswahili na
  • fasihi ya Kiswahili

33 of 37

Fasihi ya Waswahili

  • Hakubaliani na madai kuwa Waswahili si watu wote wa pwani wenye kuzungumza kiswahili bali ni zile jamii zilizoko kwenye upwa wa kaskazini kuanzia Tanga [Tanzania] hadi Barawa [Somalia]
  • Waswahili ni wenyeji wa mwambao wa A,M na visiwa vyake ambao ambao lugha yao ya mama ni Kiswahili, wenye utamaduni unaoshabihiana katika mambo mengi, ikiwemo dini ya Kiislamu
  • Kwa vile wapo, basi wanayo fasihi yao iitwayo fasihi ya waswahili. Mfano Tungo za Lyongo, nyimbo mbalimbali za kijamii kmv arusi, jando na unyago.

34 of 37

Sifa bainifu za Fasihi ya Waswahili

  • Hutunguwa/huandikwa na Mswahili asili
  • Hutumia lugha ya Kiswahili
  • Huakisi mila, na utamaduni wa Mswahili na mazingira yake na hivyo humtambulisha Mswahili
  • Huwakilisha mtazamo na falsafa ya Mswahili kuhusu maisha na ulimwengu
  • Huweza pia kujumuisha ubunifu na upekee

35 of 37

Fasihi ya Kiswahili

  • Anaunga mkono hoja kuwa fasihi ya Kiswahili ni ile iliyoandikwa kwa Kiswahili, yaweza kuelezea utamaduni wa Mswahili au la.
  • Anaunga mkono kuwa fasihi hiyo huzalishwa na makundi 4 ya wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili [rej. Madumulla]
  • Hutungwa na kuandikwa kwa Kiswahili na wenyeji au mtu mwenye asili ya eneo la A.M na kati na mwenye kuzungumza Kiswahili.
  • Wapo pia waandishi wachache wanaotokea nje ya eneo la A.M na kati ambao wamesharabu Uswahili,
  • Kwa mfano, waandishi wa Kiswahili wenye asili ya Ulaya kmv. Harold E. Lambert, Graham Hyslop, Hans Cory, Rajmund Ohly, Richard Mabala.
  • Huakisi mila, utamaduni na tajriba za Mswahili wa A.M na Kati

36 of 37

Fasihi kwa Kiswahili

  • Ni fasihi iliyotokana na tafsiri za fasihi za kigeni katika Kiswahili
  • Tafsiri ya mataifa mengine kwa lugha ya Kiswahili
  • Imechochewa na kuenea kwa Kiswahili ndani na nje ya A.M na hata nje ya bara la Afrika, maingiliano kati ya wazungumzaji wa Kiswahili na mataifa mengine.
  • Fungu la fasihi ya kigeni katika fasihi ya Kiswahili.

37 of 37

Fasihi kwa Kiswahili

  • Ni fasihi iliyoandikwa kwa lugha nyingine isiyokuwa ya Kiswahili na kutafsiriwa kwa Kiswahili
  • Huakisi mila, utamaduni na tajriba ya kule ilikotoka
  • Haimtambulishi Mswahili
  • Kwa kawaida huakisi mtazamo wa taifa/lugha chanzi
  • Tafsiri za Biblia na vitabu vingine vya kidini
  • Tafsiri ya tamthiliya mbalimbali kmv Mabepari wa Venisi, Julias Kaizari
  • Tafsiri ya hadithi za Alfulela Ulela.