1 of 25

MIPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI: UZINGATIAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI�(LAND USE PLANNING COMPLIANCE)

Photo VLUP

2 of 25

Yaliyomo

  1. Utangulizi.
  2. Malengo ya Ukaguzi wa Uzingatiaji
  3. Taratibu za Ukaguzi wa Uzingatiaji
  4. Mbinu za Ukusanyaji wa Taarifa
  5. Matokeo ya Ukaguzi
  6. Mafanikio
  7. Changamoto na Mapendekezo
  8. Hitimisho

3 of 25

Utangulizi

Mipango ya Matumizi ya Ardhi?

  • Kwa mujibu wa Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Sura 116, Mipango ya Matumizi ya Ardhi ni utaratibu ambao matumizi ya ardhi katika eneo la upangaji yanaainishwa, kusimamiwa, kufuatiliwa na kutathminiwa ili kuwa na matumizi endelevu ya rasilimali ardhi

4 of 25

Utangulizi…unaendelea

Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi

  • Ni utaratibu wa kuchunguza na kubaini ikiwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi inayoandaliwa inazingatia Sera, Sheria, Kanuni, Miongozo, Taratibu na Viwango.

Msingi wa Ukaguzi

5 of 25

Utangulizi…unaendelea

Majukumu ya Tume katika Uzingatiaji

  • Kukagua Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa Mujibu wa Kifungu cha 8 cha Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Sura 116.
  • Kuzijengea uwezo Mamlaka za Upangaji juu ya Uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi.
  • Uperembaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa mujibu wa Kanuni za Mipango ya Matumizi ya Ardhi kifungu cha 18 (1)
  • Kuratibu na kukagua Sekta zote kwa viwango vya pamoja na kumshauri Waziri kuweka viwango vilivyokubalika vya matumizi ya ardhi.

6 of 25

Utangulizi…unaendelea

Kwanini Ukaguzi wa Uzingatiaji

  • Takwa la kisheria (Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Sura 116).
  • Nyenzo muhimu ya kuthibiti (regulate) na kusimamia Mipango ya Matumizi ya Ardhi.
  • Kubaini viatarishi vinavyoweza kukabili Mipango ya Matumizi ya Ardhi wakati wa kuandaa, kutekeleza na kusimamia Mipango.
  • Kubaini mapungufu, mafanikio na kutoa mapendekezo ya namna ya kuongeza ufanisi katika uandaaji, utekelezaji na usimamizi wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi

7 of 25

Utangulizi…unaendelea

Malengo ya Ukaguzi

  • Kutambua ni kwa jinsi gani ushiriki wa wananchi umezingatiwa wakati wa Upangaji na Utekelezaji wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi
  • Kubainisha Mipango ya Matumizi ya Ardhi ilivyozingatia mahitaji ya jamii, kiuchumi, mazingira na masuala mengine mtambuka ya kisekta.
  • Kubaini vigezo vya upangaji na namna vilivyozingatiwa.
  • Kubaini ushiriki wa wadau na sekta mbalimbali katika uandaaji na utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi.
  • Kuishauri Serikali ipasavyo kuhusu masuala ya Upangaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi nchini.

8 of 25

Utangulizi…unaendelea

Utaratibu wa Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi

9 of 25

Utangulizi…unaendelea

Tathmini na Ufuatiliaji wa Matokeo ya Ukaguzi

10 of 25

Utangulizi…unaendelea

Mbinu na zana za ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa

Mbinu za ukusanyaji taarifa

  • Kupitia nyaraka
  • Mahojiano ya Kaya
  • Majadiliano ya Makundi Maalumu (FGD)
  • Mahojiano na watoa taarifa muhimu (Key Informants).
  • Uchunguzi - kutembelea uwandani.

Zana za ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa

Taarifa za msingi (primary data) na taarifa za mapitio ya tafiti (secondary data) za Mipango ya Matumizi ya Ardhi.

  • Kobo toolbox
  • SPSS,
  • Excel
  • Stata
  • QGIS

11 of 25

Utangulizi…unaendelea

Vigezo wakati wa Ukaguzi

  • Uzingatiaji wa Sera, Sheria, Kanuni, Miongozo, Taratibu na Viwango (Adherence to Policies, Laws, Regulation, Guideline, Procedures, Standards)
  • Ushirikishaji wa jamii na uwajibikaji wa jinsia katika Mipango ya Matumizi ya Ardhi (Community participation, Gender consideration and Involvement).
  • Uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Wilaya (Adherence to District Land Use Framework Plan)
  • Uwepo na uwajibikaji wa wadau mbalimbali katika Mipango ya Matumizi ya Ardhi (Stakeholder’s involvement and Integration of different sectors)

12 of 25

Utangulizi…unaendelea

Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 120

  • Mawanda (scope) ya Ukaguzi wa Uzingatiaji Vijiji 120, Halmashauri za Wilaya 69 na Mikoa 24 Tanzania Bara.
  • Kupitia nyaraka mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mipango ya Matumizi ya Ardhi.
  • Mahojiano yalifanyika kwa Viongozi wa Mkoa, Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri za Vijiji (wastani wa wajumbe 20 hadi 25 wa Halmashauri za Vijiji walihojiwa).
  • Jumla ya Dodoso 1467 zilihojiwa kwenye kaya
  • Uchunguzi uwandani (kutembelea uwandani)
  • Uchambuzi wa taarifa
  • Ripoti ya Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi

13 of 25

Matokeo ya Ukaguzi

Matokeo ya Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Vijiji 120

1. Uelewa juu dhana ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ngazi ya Kijiji (kaya)

  1. 56% zina uelewa juu ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi na 44% hazina
  2. 62% zimeshiriki uandaaji wa Mipango na 38% hazikushiriki.

14 of 25

Matokeo ya Ukaguzi…yanaendelea

2. Uzingatiaji wa maeneo yaliyotengwa kwa matumizi mbalimbali

  1. Alama zinazotumika kuonyesha matumizi; mabango 38%, Vibao 24.8%, beacons 8.1%na kupaka rangi miti 26%.

Mabango ya matumizi ya ardhi

15 of 25

Matokeo ya Ukaguzi…yanaendelea

Uwekaji wa Alama za Matumizi ya Ardhi

16 of 25

Matokeo ya Ukaguzi…yanaendelea

b) Maeneo ambayo hayajawekewa mabango ni 26.4% na katika maeneo haya matumizi yaliyotengwa hayazingatiwi.

Mabango yaliyo Ofisi ya Kijiji

17 of 25

Matokeo ya Ukaguzi…yanaendelea

3. Mahusiano ya alama na uzingatiaji wa matumizi yaliyopangwa

  1. 54% ya kaya zinakiri kuwa matumizi yaliyopangwa yanafuatwa kutokana na uwepo wa alama/mabango.
  2. 46% ya kaya zimeeleza kuwa matumizi ya ardhi ni tofauti na mpango unavyoelekeza ingawa alama/mabango yamewekwa.

4. Ushiriki katika Mipango ya Matumizi ya Ardhi

  1. Ushiriki wa wananchi katika uandaaji na upitishaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ni 62% kati ya kaya 1467 zilizohojiwa na 38% hazikushiriki katika mikutano.
  2. 56% ya Wanakijiji wanaweza kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi

18 of 25

Matokeo ya Ukaguzi…yanaendelea

19 of 25

Matokeo ya Ukaguzi…yanaendelea

5. Ukiukwaji wa Miongozo mfano; katika Halmashauri 69 zilizokaguliwa ni 68% tu ya wajumbe wa Kamati Shirikishi ya Usimamizi wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ngazi ya Wilaya (PLUM) ndio waliteuliwa kwa barua.

6. 45% ya PLUM hawana mafunzo ya uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa mujibu wa Miongozo.

7. Kutokutekelezwa kwa Mipango Kazi ya Jamii (Community Action Plans) kwa mujibu wa sekta.

8. Mipango ya Matumizi inayoandaliwa kuishia hatua ya 4 badala ya kufikia hatua ya sita.

9. Kati ya Vijiji 3874 katika Halmashauri za Wilaya 69 zilizokaguliwa, jumla ya Vijiji 1058 pekee ndivyo vyenye Mipango ya Matumizi ya Ardhi. Hii ni sawa na 27% ya Vijiji vyote.

10. Vijiji 2816 sawa na 73% havina Mipango ya Matumizi ya Ardhi.

11. Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji yaliyomaliza muda wake kuendelea kufanya kazi.

20 of 25

Mafanikio ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi

Mafanikio yaliyopatikana kutokana na Mipango ya Matumizi ya Ardhi

  • Utatuzi wa Migogoro ya matumizi ya ardhi.
  • Uongoaji wa shoroba za wanyamapori na WMA (Wildlife Management Area).
  • Urejeshaji wa uoto uliopotea na ulinzi wa maeneo ya hifadhi na biaoanuwai (biodiversity)
  • Utengaji wa maeneo ya uwekezaji
  • Kuongeza usalama wa chakula (food security)
  • Ongezeko la kipato kupitia kilimo, ufugaji, misitu (biashara ya hewa ukaa), utalii (WMA) na CSR kwa maeneo yenye wawekezaji.

21 of 25

Changamoto

Changamoto zinazokabili Mipango ya Matumizi ya Ardhi

  • Uhaba wa rasilimali fedha, watu na vifaa katika Halmashauri za Wilaya.
  • Kuongezeka kwa mahitaji ya ardhi kutokana na kuongezeka kwa watu na mifugo.
  • Elimu na uelewa wa wataalamu na wadau juu ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi
  • Halmashauri kutotenga bajeti kwa ajili ya kuandaa Mipango ya Matumizi ya Ardhi.
  • Ukosefu wa Kanzi data Vijijini na Wilayani.
  • Ukosefu wa fedha za kulipa fidia kwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya matumizi umma.
  • Halmashauri kutofanya ufuatiliaji na tathmini ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji iliyo katika Wilaya zao.
  • Ushawishi wa kisiasa (political influence).

22 of 25

Mapendekezo

Mapendekezo/Ushauri

  • Ili kuleta ufanisi na Tija ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ni muhimu utekelezaji na usimamizi wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ufanyike hadi hatua ya sita (6)
  • Halmashauri za Wilaya zisisitizwe na kuendelea kutenga bajeti kwa ajili kuandaa Mipango, ufuatiliaji na tathmini ya mipango ya matumizi ya ardhi katika vijiji ndani ya Wilaya husika.
  • Kuhakikisha nyaraka za mipango ya matumizi ya ardhi zinarudishwa Kijijini kwa ajili ya kusaidia zoezi zima la usimamizi katika utekelezaji wa mipango kazi iliyowekwa na usimamizi wa sheria ndogo.
  • Kuboresha mfumo wa utoaji taarifa ya mikutano ya vijiji ili wananchi waweze kuhudhuria kwa wingi katika mikutano hiyo.
  • Mipango ya maendeleo ya Wilaya (Halmashauri na Taasisi) izingatie Mipangokazi ya Vijiji vyenye Mipango ya Matumizi ya Ardhi.

23 of 25

Mapendekezo…yanaendelea

  • Kuanzishwa kwa vyama vya ushirika wa wafugaji (Pastoralists Cooperatives) ili kuweza kuchangisha fedha kwa ajili ya utwaaji wa maeneo ya malisho ambayo ndiyo yamekuwa changamoto kubwa katika utekelezaji wa mpango wa matumizi ya ardhi, hivyo kusababisha migogoro isiyoisha. (Sekta Binafsi za upangaji zinaweza kupata fedha za upangaji kupitia Ushirika wa wafugaji au wakulima)
  • Kuanzisha mfumo (system) wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi
  • Kutoa elimu juu ya utekelezaji na usimamizi wa mpango wa matumizi ya ardhi katika Vijiji.
  • Utekelezaji na Usimamizi wa Mipango ya Matumizi ya ardhi uwe ni agenda mtambuka katika vikao vya Halmashauri za Wilaya na Vijiji
  • Halmashauri za Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri za Vijiji ziweke utaratibu wa kuhuisha au kuchagua upya mabaraza ya ardhi yaliyomaliza muda wake.
  • PLUM ziwezeshwe mafunzo ya kuibua na kuandika miradi inayotokana na matatizo yaliyoibuiwa wakati wa uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi.

24 of 25

Hitimisho

Hitimisho

“Maendeleo ya Kidigitali ni muhimu katika Udhibiti na Usimamizi wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi nchini.

25 of 25

ASANTE SANA