DODOSO LA MAONI
Sign in to Google to save your progress. Learn more
DODOSO LA MAONI YA WADAU KUHUSU MAPITIO YA SHERIA YA BIMA ZA VYOMBO VYA MOTO, SURA YA 169

 

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania inafanya mapitio ya Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto, Sura ya 169 kwa lengo la kuiboresha ili iendane na mahitaji ya sasa ya sekta ndogo ya Bima.  Sheria  hii ni ya  muda mrefu na utekelezaji wake umeonekana kuwa na changamoto. Sheria hii ilitungwa mwaka 1945 na kuanza kutumika mwaka 1946, ikiwa na lengo la kuweka masharti ya bima dhidi ya majanga yanayotokana na matumizi ya Vyombo vya Moto. 

Ukiwa mdau muhimu wa Bima hapa nchini, Tume inakuomba kujaza dodoso hili kwa kutoa maoni yako kuhusu mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto, Sura ya 169. Lengo la maboresho hayo ya Sheria ni kulinda maslahi ya wananchi, wamiliki wa vyombo vya moto/wakatabima, makampuni ya bima na wadau wengine.

Tunatanguliza shukran kwa kushiriki kutoa maoni yako kwa sababu ni muhimu katika kuboresha Sheria ya Bima ya Vyombo vya Moto, Sura ya 169.

1. Aina ya mdau (chagua):  *
1.1. Kama wewe ni mdamu mwingine (si kati hao waliotajwa hapo mwanzo) tafadhali, jitambilishe ni mdau wa namna gani
2. Miaka ya uzoefu/ushiriki katika masuala ya bima za vyombo vya moto *
3. Mkoa/eneo unalotokea:  *
4. Je, unaifahamu Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto, Sura ya 169?  *
5. Kwa maoni yako, kiwango cha utekelezaji wa Sheria hii kwa sasa kikoje?  *
6. Ni changamoto zipi kuu ambazo umekumbana nazo katika utekelezaji wa Sheria hii? (eleza):  *
7. Je, kuna masharti katika Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto yanayokinzana na Sheria ya Bima, Sura ya 394?  *
7.1. Je, kuna masharti katika Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto yanayokinzana na Sheria ya Bima, Sura ya 394? Toa sababu *
8. Je, unaona ipo haja ya kurekebisha Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto ili iendane na Sheria ya Bima, Sura ya 394?  *
8.1. Je, unaona ipo haja ya kurekebisha Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto ili iendane na Sheria ya Bima, Sura ya 394? Toa sababu
9. Kwa mazingira ya sasa Sheria hii inaweza kusimamiwa na mamlaka/ taasisi ipi? (Eleza):  *
10. Je, adhabu zinazotajwa kwa fedha ya Pauni ya Uingereza zinafaa kuendelea kutajwa hivyo? 
Clear selection
10.1. Je, adhabu zinazotajwa kwa fedha ya Pauni ya Uingereza zinafaa kuendelea kutajwa hivyo? pendekeza mbadala
11. Je, utaratibu wa sasa wa fidia kwa waathirika wa ajali za vyombo vya moto ni wa haki?  *
11.1. Je, utaratibu wa sasa wa fidia kwa waathirika wa ajali za vyombo vya moto ni wa haki?   Toa maelezo *
13. Sera ya Usalama Barabarani inaelekeza kuwepo kwa mfumo wa fidia kwa waathirika wa vyombo vya moto kabla ya kuthibitisha kosa mahakamani (No-fault system), una maoni gani kuhusu mfumo huo? Eleza *
13. Ni changamoto zipi ambazo waathirika wa ajali za vyombo vya moto hukutana nazo wanapodai fidia?  *
14. Je, Sheria ya sasa inaakisi maendeleo ya teknolojia (mf. mifumo ya kielektroniki ya bima)?  *
15. Ni maboresho yapi ya kiteknolojia ungependekeza yaingizwe katika Sheria?  *
16. Je, Sheria ya sasa inaendana na Sera ya Taifa ya Usalama Barabarani ya 2009? 
Clear selection
16.1. Je, Sheria ya sasa inaendana na Sera ya Taifa ya Usalama Barabarani ya 2009? Eleza *
17. Kwa ujumla, ni marekebisho yapi ya kisheria ungependekeza yafanywe katika Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto, Sura ya 169?   *
Submit
Clear form
Never submit passwords through Google Forms.
This content is neither created nor endorsed by Google. - Terms of Service - Privacy Policy

Does this form look suspicious? Report