MAFUNZO ENDELEVU (CPD) KWA WATOA DAWA WA MADUKA YA DAWA MUHIMU

MADA YA PILI: MATUMIZI SAHIHI YA DAWA

Utangulizi

Kufanikishwa kwa tiba kutawezekana pale tu mtoa dawa atakapoweza kutoa maelezo

ya matumizi sahihi ya dawa.

Matumizi ya Dawa

a)    Maana ya matumizi sahihi ya dawa

Matumizi sahihi ya dawa hujumuisha mgonjwa kupokea dawa sahihi kulingana na mahitaji yake ya kiafya, katika dozi sahihi, muda sahihi wa matibabu.

b)    Matumizi ya dawa yasiyo sahihi

Matumizi yasiyo sahihi ya dawa hujumuisha; Kutumia dozi isiyo sahihi, kushindwa kumaliza kozi, kutumia dawa isiyo sahihi katika kutibu ugonjwa, kutumia dawa kwa njia isiyo sahihi, kununua na kutumia dawa kiholela bila kufanyiwa uchunguzi, kutumia dawa yenye viwango vya chini vya ubora, kutumia dawa ambayo ni ghali bila sababu ya msingi, kutumia dawa zinazoingiliana kiutendaji kwa pamoja mfano tetracycline na magnesium trisilicate, kutumia viuavijasumu (antibiotics) kutibu magonjwa yanayotokana na virusi (viral infections), kutumia dawa na pombe, kutumia dawa zisizoruhusiwa wakati wa ujauzito mfano albendazole, doxycycline, phenytoin n.k

c)    Faida za matumizi sahihi ya dawa

Kuboresha afya ya mtumiaji wa dawa, kutimiza lengo sahihi la matumizi ya dawa husika, kupunguza uwezekano wa kujenga usugu wa vimelea vya magonjwa, kupunguza madhara/maudhi ya dawa, kupunguza gharama zisizo za lazima kwa mgonjwa na Serikali, kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa yatokanayo na utumiaji sugu wa dawa, jamii kuwa na imani na dawa pamoja na mifumo ya kutolea huduma za afya .

d)    Sababu zinazochangia matumizi yasiyo sahihi ya dawa

Kutogundua ugonjwa, uandikaji wa dawa usio sahihi, utoaji wa dawa usio sahihi, mgonjwa kushindwa kumudu gharama ya dawa, mgonjwa kutotumia dawa kwa usahihi, mgonjwa kujiamulia matumizi ya dawa bila kupata ushauri wa Mtaalamu wa Afya.

e)    Mtoa dawa anaweza kuchangia matumizi yasiyo sahihi ya dawa kama atafanya

yafuatayo:

·       Kushindwa kuelewa cheti cha mganga na kuacha kuwasiliana naye ili kupata ufafanuzi,

·       kutoa dawa isiyo sahihi,

·       kushindwa kukokotoa au kutoa kiasi sahihi cha dawa,

·       kuandika lebo kwa makosa au isiyosomeka vizuri,

·       kutoa maelekezo yasiyojitosheleza kuhusu matumizi ya dawa,

·       kushindwa kuhakikisha kuwa mgonjwa ameelewa maelekezo ya matumizi ya dawa,

·       kutoa dawa au maelezo ya dawa bila kuzingatia imani,

·       mazingira au mila za mgonjwa,

·       kushindwa kuhimili shinikizo la mgonjwa la kutaka kuuziwa dawa ambayo kimsingi haiitajiki,

·       kutoa dawa kwa tamaa ya fedha bila kuzingatia ubora wa huduma,

·       mgonjwa kushindwa kumudu gharama ya Dawa.

 

Kumekuwa na tabia/kasumba kwenye jamii kwa baadhi ya watu kujiamulia kutumia dawa bila kumuona mtaalamu wa afya, hii inaweza kusababishwa na mambo yafuatayo:-

·       Kujitibu kupitia kwenye mitandao (self treatment),

·       kufuata ushauri wa mtu ambaye sio mtaalamu wa dawa,

·       matumizi ya dawa zilizobaki ambazo zilikuwa za mtu mwingine au kuhifadhi dawa kwa matumizi ya baadae,

·       mgonjwa kushindwa kumudu gharama za kumuona mtaalamu wa Afya,

f)     Athari zitokanazo na matumizi yasiyo sahihi ya dawa

·       Mgonjwa hatapata tiba sahihi na hivyo kuendelea kuugua au wakati mwingine kupelekea kifo ,

·       uwezekano wa kupata madhara ya dawa,

·       kuongezeka kwa usugu wa vimelea hii hutokea zaidi kwa dawa aina ya viuavijasumu (antibiotics) na dawa za malaria,

·       kupoteza fedha nyingi katika matibabu na mgonjwa kutegemea zaidi dawa hata kama haiitajiki.

g)    Wajibu wa Mtoa Dawa katika kuchangia matumizi sahihi ya dawa

Ili kuhakikisha dawa zinatumika kwa usahihi, Mtoa Dawa anapaswa kufanya mambo yafuatayo:-

·       Kugundua kwa usahihi dalili za ugonjwa,

·       kutoa rufaa kwa mgonjwa kwenda ngazi inayohusika kulingana na mahitaji ya kiafya,

·       kumpa mgonjwa dawa sahihi kulingana na cheti cha daktari au maelezo ya mgonjwa na kutoa maelekezo kwa mgonjwa juu ya matumizi na uhifadhi sahihi wa dawa nyumbani.

Sign in to Google to save your progress. Learn more
Namba ya Usajili *
Andika namba yako ya Usajili (PIN)

MASWALI

Chagua herufi ya jibu sahihi katika maswali yafuatayo;

1.    Mambo yanayoweza kuchangia mtoa dawa kushindwa kutoa dawa kwa usahihi ni pamoja na;

*
2 points

2.    Vimelea vinaweza kuwa sugu kwa makundi yafuatayo ya dawa;

*
2 points

3.    Ili Mtoa Dawa aweze kutekeleza kazi zake anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo isipokuwa

*
2 points

4.    Mtoa dawa anaweza kuchangia matumizi sahihi ya dawa kwa kufanya yafuatayo;

*
2 points

5.    Lipi kati ya yafuatayo huchangia matumizi sahihi ya dawa ?

*
2 points

6.    Ipi kati ya zifuatavyo ni faida ya matumizi sahihi ya dawa?

*
2 points

7.    Umuhimu wa kutoa dawa kwa cheti cha mganga ni pamoja na;

*
2 points

8.    Mtoa dawa anaweza kuchangia matumizi yasiyo sahihi ya dawa kama atafanya yafuatayo;

2 points
Clear selection

9.     Mgonjwa anaweza kusababisha usugu wa vimelea kwa kufanya yafuatayo Isipokuwa;

*
2 points

10.    Ipi kati ya zifuatazo ni siyo athari zinazoweza kusababishwa na matumizi ya dawa zilizobaki kwa matumizi ya baadaye;

*
2 points
Submit
Clear form
Never submit passwords through Google Forms.
This content is neither created nor endorsed by Google. - Terms of Service - Privacy Policy

Does this form look suspicious? Report